Friday, May 24, 2013

Discovering Your Talent and Potentials....In A Soul Breakfast

Siku Ya Kesho ya Jumamosi nitakuwa Chuo Cha Ardhi Nikiongea na wanafunzi na vijana kuhusu Namna gani unaweza gundua Kipaji Chako na Vipawa ambavyo Mungu ameweka ndani ya Mwanadamu.

Ni Ukweli usiopingika kuwa wengi wetu tunavipaji lakini hatujui hasa kama ni kwa ajili ya nini, wengine wana  vipaji vingi lakini ajabu hawajajua kipi kitawatoa, wengine hawajui kabisa kama wanavyo. Ni ukweli usiopingika kwa sasa wengi wanaacha kazi walizonazo na kugeukia talents zao ili kuweza kutimiza kusudi la wao kuumbwa kwao. Your destiny ina Connection Kubwa sana na Talent uliyonayo ndani yako. Mungu alijua ili uweze kutoka unahitaji kuwa na talent ndani yako. Unaweza usielewe sana lakini kwenye formula ya Mungu alianza kumpa Mtu akili kwanza kabla ya shule. Na kwenye mfumo wa Mungu akili imeshikamanishwa na talent uliyonayo.

Program itaanza saa 3 mpaka saa 6. Kwa mawasiliano zaidi wasiliana nasi kwa 0712 517284


Exposed From Facebook.....Pastor Matthew Sasali na Mwanzo Wa Huduma Yake

                                Kanisa Ambalo Pastor Matty alianzia huduma
                                          
Kuna Watu ambao Huwa mara zote huwa wananipa hamasa ya kusonga mbele kila ninapokumbuka walipopita wanapopita na determination waliyokuwa kwenye maisha. Mmoja wa watu wanaonipa sababu ya kukomaa kufanya kile ninachojisikia kukifanya kwenye maisha ni rafiki yangu, ndugu yangu na mdogo wangu wa damu ambaye ni Mchungaji Matthew Sasali a.k.a Pastor Matty ni mdogo wangu anayenifata kuzaliwa baba mmoja mama mmoja. Baba yangu ni Mchungaji, Mdogo wangu Pastor Matty ni Mchungaji, amemuo Rebecca Sasali ambaye nae ni Mtoto wa Mchungaji, Mdogo wangu wa 3 ni Joel Sasali na nne ni ni Happyness Sasali Wa Lwendo ambaye pia ameolowa na Lwendo Joshua Wa Happyness ambaye ni mtoto wa Mchungaji Lwendo.
Pastor Matthew akiwa na Baba Mzazi Mch. Sasali Senior.


Pastor Matty tumekuwa wote mini, yeye na Tumaini Mwanja tumekuwa wote chumba kimoja tumesoma wote shule ya Msingi. Alipomaliza form 4 Pastor Matty pale Makongo enzi za Kipingu, Afande Chacha na Afande Miraji akafanya vizuri akaenda kusoma Milambo Secondary huko ndipo akakutana na Prosper Alfred Mwakitalima. Alipomaliza Milambo akafanya vizuri akawa anafanya mpango wa kwenda udsm akapata Scholarship ya kwenda UK kufanya exchange program ya mwaka mmoja kisha angepata fursa ya kusoma chuo Kikuu huko huko. Tukiwa kwenye process za kwenda kushughulikia visa yake hiyo wiki alikuwa hayuko excited kiivyo, siku hiyo usiku akaamka usiku akawa anafanya maombi muda mrefu sana, alipoamka asubuhi akaniambia "Bro Siendi Tena Uingereza" nikamwambia we mzima kichwani??ok hauendi unaenda wapi??akasema anataka mtumikia Mungu, amesikia Wito wa kuwa mtumishi, nilimshangaa sana. Ukweli hakuna mtu ambaye kwenye familia aliyempa support hata baba ambaye nae ni mchungaji hakumpa support. Term ya kwanza kwenda chuoni Dodoma Bible Collage alijitafutia ada mwenyewe. Baadae nilijipa faraja kuwa atakuja kuwa msaidizi wa baba pale kanisani. Ajabu mwaka 2005 mwezi April, nikiwa chuo Kikuu alitangaza kuanza huduma kujitegemea maeneo ya mkoani Morogoro. Siku moja nikaenda sehemu aliyoanzia huduma. Ukitazama Picha hapo juu ndipo ambapo Pastor Matty alianzia huduma kwenye club ya Pombe za Kienyeji. Nilipofika nilitoka machozi kama mwanadamu nikamshangaa sana dogo ajabu yeye akawa ananishangaa mimi wakati yeye ana amani. Nakumbuka siku hiyo tulisali watu wanne, mimi yeye na wanafunzi wawili wa SUA. Nikiwa chuoni boom niliyokuwa napata ndio nilikuwa na msupport dogo angalau awe na chakula chake mwenyewe. Baada ya Miaka 3 akajenga Kanisa lenye uwezo wa kubeba watu 350. Nakumbuka mara kadhaa ilinilazimu kutoka Mzumbe Mimi, Tumaini Mwanja, Delphinus RwegasiraEdna Luvanda na Godwin Protace kwenda kumtia moyo Pastor Matty. He started from nothing, miaka michache iliyopita akahamishiwa Mkoani Mbeya ambako anatumika huko sasa na familia yake. Nikikumbuka tulipotoka utotoni, alikopita na kuanza huduma pale Morogoro ajabu ya Mungu alipoanza huduma nami nikawa chuo nilipomaliza nae baadae akahamia Mbeya...God's Ways are Zigzag.

Pastor Matty alipoanza Huduma ilimlazimu awe anapiga Kinanda na Gitaa na Kuimba yeye mwenyewe kwenye Ibada.

Kila Mtu Mungu amemuita kwa namna yake, usiudharau Mwanzo mdogo, anza pale ulipo na uanze kile ulichonacho huwezi Jua Mungu amekusudia nini katika maisha yako usisubiri uwe na hakika na kila kitu ndipo uamue. Imani ni kuwa na hakika. Chukua hatua ya Imani Mungu hatakuacha kamwe. Usimdharau Mtu ambaye Mungu ameweka ndoto ndani yake unaweza dharau leo yake kumbe hujui kesho yake, Mungu wetu ni mwaminifu sana nimemwona kwenye maisha yangu na watu wanaonizunguka.

Pastor Matthew akiwa na Mentor wake Askofu Mkuu wa Tanzania Assemblies Of God  Dr. Barnabas Mtokambali. Wakati Matthew anaenda kuanza huduma Morogoro hakuwa na nyumba ya Kufikia ndipo alipoomba ajihifadhi kwa muda katika nyumba ya Askofu Mkuu.

Picha iliyoambatanishwa ndipo Pastor Matty alipoanzia huduma yake ya Utumishi. Nikija nitaandika Kuhusu Tumaini Thomas Mwanja Mtu tuliyesoma wote ingawa sio shule moja shule ya Msingi Mpaka chuo Kikuu na kuanzisha Kampuni yetu ya Kwanza T & S Gospel Promotion mwaka 2003 (T for Tumaini and S for Samuel).

Pastor Matthew akiwa Mbeya Kwa sasa kwenye Utumishi

Pastor Matthew akiwa na Mke wake ambaye alikubali kuolewa na Kijana anayeanza Utumishi katika Club ya pombe na ku-resign kazi yake akiwa kama MD.

Pastor Matthew akiwa na gari anayoendesha kwa sasa
Pastor Matthew akiwa katika Malezi
Rebecca akiwa na Watoto Wao.


Thursday, May 23, 2013

Chesco Kilemile Kuachilia Albam Yake


Muimbaji Chesco Kilemile
DAR ES SALAAM,Tanzania
Msanii wa nyimbo za Injili, Chesco Kilemile, yupo mbioni kuachia albamu yake ya pili itakayokwenda kwa jina la  Usipoteze muda.
Akizungumza na mwandishi wa blog hii, Kilemile alisema kuwa albamu hiyo ataiachia Agosti , mwaka huu ikiwa na jumla ya nyimbo sita.
Kilemile alisema kuwa mpaka sasa amefanya video mbili za nyimbo zilizomo katika albamu hiyo na kueleza kuwa mipango yake ni kumaliza kurekodi video za nyimbo zote ili uzinduzi huo uende sambamba na DVD.
Akizungumzia waimbaji watakaomsindikiza katika uzinduzi huo Kilemile alisema kuwa ni pamoja Emanuel Mpeta na ambapo wengine bado anamaliza nao maongezi ya makubaliano ili nao waweze kumuunga mkono.
Albamu hiyo itakuwa na nyimbo kama Mambo kwa yesu, Moyo, Usipoteze muda,Ametenda, Usinipite na utabaki kwa mungu.

Sauti Za Sifa


Moving Forward Concert.....


Jitambue Ya Chris Mauki.....SABABU MBOVU ZA KUINGIA KATIKA MAHUSIANO/NDOA (Fahamu kwanini wengi hujuta baada ta muda mfupi)

Lengo la kuingia kwenye ndoa, liwe zuri au liwe baya ndilo litakalotegemeza aina ya maisha yenu katika ndoa hiyo kuwa ya furaha au ya machungu. Baada tu ya kuoana na huyo mtu wako kwa sababu zisizo za msingi, siku, miezi au miaka siyo mingi utaanza kuchoka na kutamani kutoka nje ya hiyo ndoa kwa maana baina yenu hakuna muunganiko wa ndani (emotional attachment) baina ya wanandoa wawili. Na mara nyingi hali hii hupelekea msongo wa mawazo (stress), mfadhaiko wa moyo na kukosa furaha ndani ya ndoa. Na matokeo ya hali hii kumfanya mwanandoa mmoja au wote wawili kuanza kutafuta kutoshelezwa na kuliwazwa nje ya ndoa na hapa vinazaliwa vitu vingine kama uzinzi, kutengana, talaka au magomvi na mifarakano isiyoisha.

Wanandoa wengi hawajui nini wafanye, nini waelewe ili kufanya ndoa yao zifanikiwe. Thamani ya ndoa na jinsi ndoa inavyochukuliwa sikuhizi ni tofauti sana na nyakati za wazazi wetu, na hii imewafanya wengine kujikuta wako wenye ndoa kwasababu mbovu na hivyo ndoa nyingi kuvunjika au kuyumba baada ya muda mfupi tu. Vitu kama kudhamiria, heshima na uaminifu sio vya maana tena siku hizi, sababu watu wanaogopa kuonekana wazamani na washamba.

Mtazamo wa ulimengu juu ya ndoa umeharibiwa na magazeti, luninga na vitabu mbali mbali. Siku hizi kuishi bila ndoa ni kitu cha kawaida, kuwa na mpenzi nje ya ndoa sio kitu cha ajabu tena, mapenzi nje ya ndoa sio ya kushangaza hata kidogo. Kinyume chake ukionekana kuyashangaa haya, jamii itakushangaa wewe kwa jinsi ulivyo nyuma ya wakati. Mambo yamebadilika sana, zamani binti akikutwa bikira wakati anaolewa ilikuwa sifa kwake na familia nzima, siku hizi binti akikutwa bikira atachekwa, na watu kumshangaa wakihisi ana matatizo fulani. Hali kadhalika kwa kijana wa kiume aliyejitunza. Kwa bahati mbaya sana tunaishi katika jamii ya ajabu isiyoamini katika kujitoa kwa kweli na kudhamiria katika mahusiano. Jamii isiyoamini katika uaminifu, na ndiyo maana magomvi mengi hutokea pale simu ya mmoja inapoguswa. Kuwindana na kuchunguzana kumekuwa kawaida, maadili sio jambo la kuzingatiwa tena. Wanandoa wengi ni wale wenye majeraha ya moyoni na walio umizwa, kwa hiyo hutoka nje ya ndoa zao wakitafuta mwingine aliyeumizwa kama wao ili waliwazane.



1. Hofu ya umri kupita na kuzeeka
Wako wengi sana, hususani watu wa wajinsia ya kike ambao wamejikuta wakiwakubali wanaume wa aina yoyote ili mradi tu nao waolewe maana umri wao ulionekana kusonga sana na hofu ya kutoolewa kutanda. Mwanaume anayehusiana na mwanamke mwenye tabia hii huulizwa au kulazimishwa kila siku kwenda kujitambulisha kwa wazazi wa binti au kutangaza ndoa. Ndoa nyingi za aina hii zimeishia kenye talaka na kutengana.

Wako wengine ambao kwasababu wanakiu sana ya kupata watoto na wameogopeshwa sana habari kwamba wana weza wasipate watoto kwa sababu ya umri wao, basi watacheka na kaka yeyote yule ilimradi tu waolewe au wazae naye. Wengine wajinsi hii wamejuta sana baada ya kujikuta kuwa waliyezaa naye hakuwa BABA bali mwanaume tu, tena kirukanjia tu na kwahiyo wanawake hawa wameishia kulea mtoto au watoto wao wenyewe pasipo mzazi wa pili (single parenting), jambo ambalo kwa kiasi kikubwa linawaathiri watoto wengi. Kwa wale wanaokimbilia kuolewa ili wakazae watoto, kukumbuka kuwa hata huko kwenye ndoa kuna waliokosa watoto.



2. Kuingia katika ndoa/mahusiano kwa lengo la kusaidiwa au kuongeza kiwango cha kiuchumi ulicho nacho.
Hapa wengine wamewageuza wapenzi wao kuwa mitaji au rasilimali ya kuwaondoa wao pamoja na ndugu zao kutoka kwenye umasikini. Kwa kuthibitisha hili wengine wamepewa majina kama BUZI, ATM n.k.

Katika penzi la namna hii hakuna mguso au muunganiko wa kuhisia (intimacy) baina ya wapenzi, bali kinachowaunganisha pekee ni kile kilicho mfukoni au vile vinavyoshikika na kuonekana tu. Athari za penzi la aina hii lina fungua milango mingi kwa wahusika kutokuwa waaminifu na hata kujihusisha na mapenzi nje ya mahusiano yao.


3. Kuingia kwenye ndoa sababu ya mimba au mtoto aliyepatikana kabla ndoa
Lazima kutofautisha kuwa sababu iliyowapelekea kuzaa mtoto siyo itakayowapelekea kuoana. Acha sababu ya kuoana kwenu iwe penzi lenu la dhati na sio mimba au mtoto. Suala hili linahitaji pia wazazi wajue kwamba kitendo cha watoto kupeana mimba au kupata mtoto hakitoshi kuwa sababu ya kuwalazimisha kuoana, maranyingi wazazi wamewalazimisha watoto wao kuingia katika ndoa sababu ya mimba au mtoto na kujikuta wanawaharibia maisha yao mazima. Yanini kujiingiza katika mahusiano yakudumu kisa umempa au umepewa mimba na kuifanya hiyo ndio sababu ya kulazimisha muishi pamoja kama mume na mke wakati kabla ya mimba hiyo hakuna mmoja kati yenu aliyewahi kuwaza kuwa siku mmoja mtakuwa mume na mke, badala yake baada ya kipindi kifupi mnagundua kuwa hakuna penzi baina yenu bali kinacho waunganisha ni mtoto pekee. Maumivu na vikwazo baina yenu vinawadhihirishia wazi kuwa ninyi wawili hamkutakiwa kuwa pamoja bali mmelazimisha tu. Kinacho fuatia hapo ni kufungulia mlango penzi lingine nje au kufanya mkakati wa kusitisha mahusiano yenu ili kuitafuta furaha ya kweli sehemu nyingine.


4. Kulazimika kuingia kwenye ndoa au mahusiano ya kudumu kwasababu ya upweke, (Loneliness).
Mara nyingi mtu anapokuwa peke yake (single) huwaza kuwa ndoa ndiyo inayoweza kuwa utatuzi mkubwa wa matatizo yake. Nakubaliana na ukweli wa maandiko kwamba “Sio vema mtu awe peke yake…” lakini ni vizuri tukijua tofauti iliyopo baina ya kuwa peke yako na upweke. Hivi ni vitu viwili tofauti: kuwa peke yako inamaanisha kukosa mawasiliano au ukaribu na watu wengine, unakuwa kama uliyetengwa (being alone), wakati upweke (loneliness) inahusisha nafsi, akili na hisia (soul, mental and emotions) kuwa pweke au kujihisi kutengwa na hii ni ngumu kuishuhulikia. Ni heri kuwa peke yako (single) kuliko kuwa kwenye ndoa na bado ukajisikia upweke (lonely). Wako wengine waliodhani ndoa ni suluhisho la upweke waliokuwa nao na mara walipoolewa au kuoa, mawasiliano baina yao yakayumba na hivyo kukomaza upweke kwa wote wawili (Not alone but lonely).


5. Kuolewa au kuoa kwasababu ya shinikizo kutoka kwa wazazi, ndugu au marafiki
Shinikizo hizi zaweza kuwa za kihisia au hata kihalisia. Kihisia ni pale ndugu au wazazi wanapokushawishi mara kwa mara kuoa sababu umri wako unaonekana kwenda na wako wazazi wengine husisitiza kuwa wanataka wajukuu (utasikia mzazi anasema unataka nife sijawaona wajukuu zangu?). Hata kama huhisi kulazimishwa lakini kwa kule kurudia rudia kwa kukumbushwa kila siku kunaweka shinikizo ndani yako, kunaathiri hisia zako na kuweza kukupelekea kuingia katika ndoa isiyopangiliwa. Shinikizo la kimwili au kihalisia ni pale wazazi wanopolazimisha watoto wao kuoa au kuolewa na watu fulani kwa sababu tu ni marafiki zao (family friends) au kwa sababu ya kulinda utajiri na matarajio yoyote binafsi. Ndoa nyingi za aina hii zimekuwa kero na dimbwi la maumivu na machozi, baada ya muda kidogo mna jikuta mali mnazo, wazazi wenu wanapatana na kupendana, lakini nyie kama wapenzi ni maadui wakubwa. Jiulizeni mnaingia kwenye mahusiano kwa furaha yenu au ya wazazi wenu?


6. Kuamua kuoa au kuolewa ili kupata uhuru.
Hii hutokea sana kwa wale waliozoea kubanwa sana na wazazi katika kila wafanyacho hususani katika maamuzi. Wengine huzikimbia familia zao maana hazieleweki, hazina mpangilio na hivyo kutamani kutoka ili wakaanzishe zakwao wenyewe. Kinadada na kinakaka wanachoka kuamuliwa na kuwekewa masharti ya kuvaa, kula, kufanya mambo, kutoka na kurudi kwa muda kwahiyo wanadhani ndoa ndio itawachomoa kifungoni hapo. Ninaushahidi wakutosha wa baadhi ya ambao walikimbilia katika mahusiano ili kuwa huru na kwa bahati mbaya waliyoyakuta huko kwenye mahusiano yaliwafanya watamani hali waliyoiacha nyumbani kwao ingawa kwa bahati mbaya wakati huo ‘it was too late’.




Wednesday, May 22, 2013

Tamasha Kubwa La Muziki Wa Injili Kurindima Ndani Ya Diamond Jubilee

Kanisa La KKKT Usharika Wa Tabata Segerea Wanakusudia Kuandaa Tamasha Kubwa la aina yake litakalofanyika katika Ukumbi maarufu wa Diamond Jubilee siku ya tarehe 26 May, 2013 na tamasha hilo litaanza majira ya saa 9 Alasiri Mpaka saa 1 Usiku.

Blog hii kwa hisani ya Chomoza Ya Clouds Tv ilifanya mahojiano na Mchungaji wa Usharika, Mwenyekiti wa Maandalizi na Event Coordinator Mr. Emmanuel Kwayu Kwa ajili ya Kupata maelezo ya Kina Kuhusiana na Tamasha Hilo.Mchungaji Wa Usharika huo Mch. Noah Kipingu alieleza Blog hii kuwa Makusudi hasa ya Tamasha hilo ni Kukusanya Fedha kwa ajili ya Ujenzi wa Nyumba Ya Bwana Yenye Hadhi ya Kuheshimika kama ambavyo wanadamu wamekuwa wakijenga nyumba nzuri kwa ajili yao wenyewe.

Mr. Kwayu akiongea na Blog hii aliiambia kuwa Wanamuziki watakao kuwepo siku hiyo ni Solomon Mkubwa Kutoka Kenya, Joshua Mlelwa alimaarufu kama BAM BAM, Martha Mwaipaja, Kwaya Ya Lulu na Kwaya Wenyeji Ya Tabata Segerea. Kiingilio kwa ajili ya Tamasha hilo ni sh. 10,000 kwa 5000 tu.

"Papa Hakuwa Anakemea Mapepo"- Msemaji wa Vatican


"The Holy Father did not intend to perform any exorcism," Vatican spokesman Federico Lombardi, said after the claims by TV 2000, which is owned by the Italian bishops' conference.
"As he often does with suffering people presented to him, he simply intended to pray for the suffering person," Lombardi said.
The channel quoted exorcists saying there was "no doubt the pope was either reciting a prayer for freeing from the devil or performing an exorcism".
The footage shows the pontiff laying both hands on the boy's head during a Pentecost ceremony on Sunday.
TV 2000, which has previously aired claims that the pope's predecessors, John Paul II and Benedict XVI, also "exorcised" the devil, is to broadcast a special programme on Friday devoted to "the pope's struggle against the devil and his seductions".
Exorcism is an ancient practice of driving out demons but is treated with scepticism by many Christians.
Source: Sowetanlive.

Step Up.....Sipho Makhabane: Gwiji la Muziki wa Injili aliyeishi kama kibarua mashambani.


SIPHO Makhabane si jina geni katika tasnia ya muziki wa injili barani Afrika.

ukifananisha na majina ya wanamuziki wengine kama Joyous Celebration ama Sfiso Ncwane, Rebecca Malope yeye ni mmoja wa magwiji wa uimbaji nchini kwake Afrika ya kusini akiwa ameshiriki katika shughuli mbalimbali za kiroho na kijamii.
Makabane mwenye umri wa miaka 45 amekuwa akisifika na kuvutia mashabiki wake kwa mtindo wa nyimbo zake na uchezaji.

Gwiji huyo wa muziki wa injili alitangaza kustaafu uimbaji mnamo mwaka 2010 ingawa mwaka jana alitoa albamu nyingine mpya akiwa ana miliki kampuni kubwa inayotoa wanamuziki wapya kila kukicha ya "Big Fish".

Historia yake inaeleza kuwa aliacha shule akiwa darasa la tano kutokana na ugumu wa maisha na kuamua kufanya kazi katika shamba la miwa la Kaaruls huko Mpumalanga ili aweze kuwasaidia ndugu zake na mama yake ambao walikuwa wakimtegemea yeye.

Makabane alipotimiza miaka 17 alihamia kwenye kazi za ujenzi kwenye mbuga ya ‘Kruger National Park’ ambako alishiriki katika ujenzi wa nyumba kambini hapo.
Akiwa na miaka 21 alikuwa tayari na ujuzi wa kutosha katika kazi ya ujenzi ambapo alipata kazi Pienaar kabla kupata ofa nzuri katika kampuni ya Telkom mnamo mwaka 1986 kama fundi, huku muda wote huo akipenda sana muziki wa injili lakini pia ndio ulikuwa mwanzo wake katika biashara na kujua kwamba atatengeneza pesa nyingi kupitia uimbaji.
Akiwa na miaka 25 alifunga ndoa na mkewe ambaye kwa wakati huo alikuwa na miaka 18 hiyo ilikuwa mwaka 1990 na kuanza shughuli ya kununua na kuuza kazi za muziki ndani na nje ya nchi yake.


Lakini kwa wakati huo akifanya kazi katika kampuni ya Telkom hamu ya moyo wake ilikuwa ni kurekodi albamu yake binafsi na kufanikiwa kufanya hivyo na kuonyesha kabisa kupenda kazi ya uimbaji kuliko kuweka sawa mitambo ya simu,lakini ilikuwa shida kuwavutia wasambazaji ambao alitaka wawe wananunua kazi kutoka kwake huku wakiwa hawaamini kama ana uwezo huo wa uimbaji mpaka pale waliposikia kazi yake katika moja ya radio maarufu nchini humo ya Swazi a.k.a Ligwalagwala FM.


Mkabane alitambulishwa na wimbo wa 'Ngitinikela Kuwe' ambao ndio ulikuwa wa kwanza na mwaka 1996 gwiji huyo akaamua kujikita kwenye tasnia hiyo ya muziki wa injili na kuachana na kazi yake kwenye kampuni ya simu.
Mwaka 1996 aliachia albamu iitwayo ‘yek'intokozo’ wimbo ambao mpaka leo umeacha alama kwa mashabiki wake kwa kumtambua vyema kupitia wimbo huo.

Lakini wakati huo tayari alishatoa albamu nyingine mbili miaka ya 1993 hadi 1999 zikiitwa "THUM'UMLOLO" na "JESU ULIQHAWE".

Mwaka 1998 kupitia kampuni ya CCP Records aliachia albamu yake ya nne iitwayo "Uyigugu" iliyofanya vyema, mwaka 1999 akaachia album iitwayo "Makadunyiswe" moja ya album ambayo inapendwa sana na mashabiki.
Mwaka 2001 akaachia albamu ya Calvary ambayo iliuza kufikia kiwango cha unit 21.

Mwaka 2002 akaachia ''Akukhalwa"iliyokuwa kama albamu yake ya "Yek'intokozo" ambapo iliuza zaidi ya nakala 70,000, mwaka 2003 akaachia albamu ya ''Moya wami" ambayo pia iliuza zaidi ya nakala 70,000.

Sipho Makhbane ameshirikiana katika albamu na waimbaji wakongwe wa nchini kwake kama Jabu Hlongwane, Marehemu Vuyo Mokoena, Lundi, Hlengiwe Mhlaba na wengine wengi pia akiwa nyuma ya mafanikio ya waimbaji lukuki kama Hlengiwe Mhlaba, Ncandweni Christ Ambassadors, Shongwe na Khuphuka Saved Group, na pia akiwa mtayarishaji wa albamu za waimbaji wengi.


Mwaka 2004 aliachia albamu ya "Nkosi nghibheke" ambayo ilikuwa na vigumu kwa mashabiki wake kuchagua nyimbo zilizomo kwakuwa zote zilikuwa nzuri huku kibao cha "guyizolo" ambacho kilikuwa cha shukrani kwa Mungu ambaye huwa anamtumaini kwa kila kitu, pia aliamua kutoa albamu ya muziki tupu au ala kupitia albamu hiyo.

Mwaka 2005 aliachia albamu chini ya kampuni ya SONY/BMG iitwayo "Umuzi Omuhle" akimshirikisha mwanamama Hlengiwe Mhlaba ikimtambulisha kimataifa zaidi, kama haikutosha aliachia album yake ya 15 ''Ngiyamemeza" ikiwa ni albamu yake ya tatu kutoa chini ya SONY/BMG bila kusahau nyimbo alizokuwa akizitoa kila wakati wa pasaka na kubariki watu wengi huku kampuni yake ikiwa ni moja ya kampuni kubwa kabisa nchini Afrika ya kusini.

Amewahi kuimba jukwaa moja na waimbaji kama Kirk Franklin akipata tuzo mbalimbali kama SAMA, Crown, na nyinginezo ikiwemo kutajwa kwenye tuzo za Kora ambazo zilikuwa maarufu barani Afrika.


Tuesday, May 21, 2013

Papaa On Tuesday......Ukiogopa Stress Unaweza Jikuta Ndo Unapata Stress....Hakuna Marefu Yasiyo Na Ncha

Wahenga Walikuwa ni Watu Wa ajabu sana sijui walikuwa wanawaza nini mpaka kuwa na misemo ambayo ni relevant mpaka kwenye kizazi chetu mojawapo ya misemo hiyo ni ule unaosema Hakuna Marefu Yasiyo Na Ncha, au ule msemo wa Mbio za sakafuni huishia ukiongoni hizi zote zinakuonesha kuwa hakuna jambo lolote ambalo linadumu milele. Kwenye Biblia Muhubiri sura ile ua 3 ukianza kusoma inaeleza wazi kabisa Kila Jambo na Majira yake, Mwanamuziki mmoja akaimba nothing last forever maana Hata hili nalo Litapita.

Katika Miaka ambayo tumeishi kwa sasa tunajenga kizazi kisichoweza kuwa na passion na kitu ama hata ndoto za maisha, wazazi wetu sisi walikaa miaka zaidi ya 30 kuhakikisha ndoto zao zinatimia, akina Abraham walikaa miaka 100 kusubiri mtoto, waliosoma physics wanakumbuka aliyegundua mwanga wa bulb mpaka kuwaka alifanya majaribio mangapi mpaka mwanga wa bulb kutokea. Yamkini hata wewe pia unamfahamu mtu ambaye aling'ang'ania anachokiamini mpaka kikaja kutokea kuna mahali alikuwa anaona kitu ambacho watu wengi hawakioni anakiona peke yake, aliamini katika hilo yamkini pengine alichekwa kwa miaka kadhaa mpaka kuja kutokea uhalisia. Nimewahi kusema mara kadhaa kuwa ilimchukua mama yangu miaka kadhaa kuja kunipata mimi kama mtoto wa kwanza, sikupewa tu jina la Samuel eti sababu ni zuri la hasha lina langu lina maana kubwa sana kwa wazazi wangu. Kile kipengere cha kwenye ndoa cha kusema katika hali njema ama mbaya, katika umasikini ama utajiri siku hizi nasikia kime expire maana watu wanapenda hali njema peke yake na wakati wa utajiri wakati wa kufanikiwa tu wakati wa shida watu wanasahau hata hilo nalo litapita.

Miaka yetu kimeibuka kizazi cha soft touch kizazi cha google kizazi ambacho hakipendi shida, kizazi ambacho hakiwezi suffer, kizazi kisicho na uvumilivu. Ukionana na waajiri watakuambia kiwango cha waajiriwa wanaoacha kazi kinakuwa kila iitwapo utasikia mtu amesema "mie nimeamua kuacha kazi wananifatafata" yaani kwa akili yake ilivyo safi anaona bora alale nyumbani kuliko kufanya kazi kwenye manyanyaso, mwingine utamsikia "nimeamua kumpiga chini boyfriend wangu hasomeki",yaani sikuhizi kama haueleweki unaachwa hapo hapo, kama ni kwenye nyumba zetu za Ibada kila mtu anasema anahamia kwingine sababu huku kwingine wako shallow. Mtu akipata swali gumu ama kitu kigumu ana google, enzi zetu sisi google tunaijulia wapi? hesabu unabeba mpaka visoda na vijiti mpaka ujue table ya 9, Viboko ilikuwa ni sehemu ya mambo yaliyotukuza na kutusababishia tuwe kama tulivyo watoto wa siku hizi hawachapwi wana sheria zinawalinda. Hiki ndicho kizazi ambacho mwanaume akiona hawapati watoto anaamua kwenda kutafuta nje ya ndoa, hiki ni kizazi cha Watu wanaojua kila jambo hakuna ambaye hajui ukifanya cha kwako atakuambia tu 'pale umekosea kidogooooo ungefanya hivi....... Sisi ndio kizazi ambacho leo unaweza anza kuuza maandazi, kesho unahamia ubuyu kesho kutwa rambaramba, ni nani yuko tayari kutoboa na jambo mpaka kieleweke.

Siku hizi kuna course za Stress Management wakati tunakuwa hizi kozi hazikuwepo, Stress Zimezidi mpaka watu wanafundushwa namna ya kuzimanage Stress, Ukiwa Single kuna Stress, Ukikaribia Kuoa Stress, Ukioa Stress, Ukiwa kazini  Stress, Ukirudi Nyumbani Stress, Stress is everywhere hata mwalimu wa Stress Management nae ana Stress. Umewahi kujiuliza kuwa kwanini Una Stress??Umewahi kujiuliza kwanini Kizazi hiki fundishwa Stress Management??Mwalimu wangu wa Saikolojia wakati nasoma alisema kuna Chronic Stress na Normal Stress na akasema stress is unkwepable yaani lazima kila mwanadamu kwa asili awe stressed sasa level na frequent of stress ndo huwa unapelekea kuwa common ama normal, hata kuamka asubuhi na kupanda daladala kuna stress zake, stress everywhere nilimuuliza mwalimu wangu wa Stress Management akiwa Stressed yeye huwa anaaenda wapi kupunguza Stress zake??kumbe mganga hajigangi. Kwa sababu ya Stress watu hawapendi Stress ndo maana kizazi chetu utasikia Sipendi Stress Nimemuacha. Hakuna ambaye yuko tayari kulivumilia jambo likatokezea upande wa pili.

Hakuna jambo linadumu kwenye maisha ya mwanadamu milele na milele, kuna nyakati unakataliwa na ndugu jamaa na marafiki, kuna wengine wetu tuliwahi tengwa na ndugu kwa sababu tulitolewa juu tukaja zero kabisa. Kuna wengine wametengwa na ndugu kwa sababu uwezo wao wa kiuchumi ni mdogo, kuna watu wanadharauliwa kwa sababu kadha wa kadha Hakuna marefu yasiyo na ncha hata hilo ulilo nalo litapita. Leo unaweza kuona Papaa amevisha mtu pete ukadhani ilikuwa ni rahisi, muulize Paul kwenye Biblia atakuambia Vita amevipiga, Imani ameilinda na Mwendo ameumaliza alikuwa anamaanisha nini. Wachache wetu kwneye kizazi hiki wako tayari kupambana na ndoto zao mpaka zitoke halisia. Watu hawapendi stress kwanini aumie??Sisi ni Kizazi kinachopenda mambo ambayo yako tayari tayari (readymade things). Wachache wanapenda kulifanya jambo likatokea, vijana wengi wanakuambia "mie nimemwacha hajatulia". Unataka ambaye ametulia kabisaa, basi wengine wetu leo tusingekuwa hapa tulipo, wengi wetu tumepishana na kuwapoteza wale waliokuwa wawe wenza wa maisha yetu kwa sababu tu "wanaonekana hawajatulia". Unajisikiaje pale ambapo umemwacha mtu kwa kudhani hajatulia, halafu akatokea risk taker mmoja akaamua "kumtuliza mtu". Sasa usije ukakurupuka ukajifanya risk taker kwa tamaa zako utasoma namba kwenye maisha yako, utasubiri sana rolling ya wimbo na usiipate. Nuru huwa inafaa sana gizani na sio kwenye mwanga wa jua. Kama wewe ni Nuru ya Ulimwengu basi tafuta giza na uoneshe Nuru yako. Yesu alimtuliza Sauli aliyekuja kuwa Paul ambaye hakuwa ametulia, Yesu alikutana na Mwanamke Msamaria aliyekuwa hajatulia, akamtuliza. Ninampenda Sana Yesu kwa sababu anaichukua Raw Material na Kuifanya Kuwa Product ingawa hiyo Process Sio Ya Kitoto...waliosoma Processing Industry Engineering Watakubaliana na mimi kuwa kwenye Process ndo kuna kukamilishwa. Nakumbuka Wakati ninaanza uhusiano na Milembe wangu watu kibao walienda kwa Milembe, OOh unajua Papaa hajatulia, oooh Unajua Papaa hasomeki, Unajua Papaa ana mambo mengi, jambo moja ambalo alilijua hii ni Project amepewa na na Mungu kufanya aliyekuwa hajatulia kutulia, anayeonekana hafai kuwa dhahabu ya kesho, kutoka kwenye kukataliwa kwenda kwenye kufaa, sasa wewe unadhani lile goti mtu mzima nilipiga sababu tu mazoea?jambo usilolijua ni kama usiku wa giza, ajabu kubwa wale wale waliokuwa wanaongea mwanzo ndo hao hao wanakuja aisee hongera, Mungu kweli ni Mkuu, Mungu kweli anaweza....utabaki kuwaambia wenzako, unless uamue ku-practice kile ambacho Mungu anasema na wewe kwenye maisha yako.

Maji ukiyavulia nguo huna budi kuyaoga kama umeamua kufanya biashara halafu unaamka saa 4 basi jua una shida mahali, kama umeamua kujiajiri lakini unasubiri simu za watu ili wakupe ma-deal basi jua utarudi kijijini hivi karibuni, kama umeamua kuajiriwa halafu saa za kazi ndo unatumia vibaya basi subiri punguzo la wafanyakazi linakuja. Kila Jambo lina majira yake chini ya jua inawezekana leo huna lakini hakuna kilicho zaidi ya hakuna from hakuna ndo kuna kuwa nacho. Ukiona mambo yanakutokea jiulize kwanza maswali je mimi niko safi??kabla sijarushia mpira kwa wengine, ukiona uko safi na bado hakieleweki tafuta msaada. Unaweza ukawa unapata tabu bure kumbe unachopitia wenzako 1000 wameshasaidiwa na kupata msada na kusonga mbele. Yamkini tabia yako ndio imekuwa chanzo wewe kuwa hivyo ulivyo umewahi jihoji??

Hakuna Marefu Yasiyo na ncha, Hata Hilo Nalo Litapita. 

Ze Blogger
0713 494110

Monday, May 20, 2013

Revival Flames Praise and Worship Season 1


Watu Wanne Wapoteza Maisha na 30 Wajeruhiwa Kwa Sababu Ya Anointed Water Ya Tb Joshua.



FOUR people died and 30 others were injured Sunday in a stampede in a popular church in Ghana, caused by an offer of free anointing water, police said.
Thousands of worshippers hoping for water that they believe can cure illnesses gathered at the Nigerian prophet T. B. Joshua's Synagogue Church of All Nations in the capital Accra, when people in the back began pushing to get to the altar.

"In trying to get it, a stampede happened," said police spokesman Freeman Tetty. "Four are confirmed dead and 30 are injured, some in critical condition."

One worshipper, Gertrude Sumbamala, who suffered a broken leg in the incident, had travelled from Ghana's far northwest for an interview for a job promotion, then decided to go to the church.
"We went there as early as four" in the morning, she said.
"People from the back, they pushed... and they fell on us. So we were battered by a lot of forces."
Innocent Adraku said her mother was also trampled by the crowd, and was admitted to the hospital with chest pains.
"We also came to receive the anointing water, that was all," said Adraku whose mother travelled from the regional capital Ho near Ghana's border with Togo.
The police spokesman said an investigation into the stampede had been launched. No arrests were made.
Reverend Sam McCaanan told local radio station Citi News that a planned service had been cancelled.
"We are used to numbers," he said but such an incident was unprecedented.
"We are devastated, it's very unfortunate and we are very sorry," he added, promising to make sure this does not happen again.
Joshua commands one of the continent's largest evangelical Christian denominations from his base in Lagos.
He is known for his prophecies about world events and for performing what his followers consider miracles, like curing blindness.
West Africa's second largest economy with a population of 25 million, Ghana is predominantly Christian, with evangelical Protestant churches like Joshua's being a particularly popular segment of the religious landscape.

Askofu Dr. Moses Kulola Alazwa Hospitali Ya Bugando





Tukiwa kama Mwili Wa Kristo tunayo haja ya Kuunganisha Imani Zetu na  popote ulipo kumbuka kumuweka katika maombi Askofu Mkuu wa kanisa la Evangelistic Assemblies of God Tanzania (E.A.G.T) Dkt. Moses Kulola ambaye amelazwa katika hospitali ya Bugando jijini Mwanza akipatiwa matibabu ya kiafya

Askofu Kulola na mmoja wa wajukuu zake akiwa hospitalini kwa matibabu.

Picha kwa hisani ya Flora Mbasha habari kwa Hisani Ya Gospel Kitaa

Kundi la Glorious Worship Team a.k.a GWT kufanya Ziara Nchini Kenya



Lile Kundi Maarufu la Glorious Worship Team linatazamia kufanya Ziara katika Nchi ya Kenya katika maeneo ya Mombasa, Nairobi na Eldoret kwa ajili ya Kutangaza jina la Yesu.

Kupitia Kipindi cha Gospel Hits ya Tv Sibuka na Chomoza Ya Clouds Tv Viongozi wa Kundi hilo wameutaarifu umma wa Watanzania kuwa Ziara hiyo inayotazamia kuanza rasmi Alhamis wiki hii itawachukua wiki 2 kabla ya Kurudi Jijini Dar na Kisha Kurudi tena nchini Kenya kuendelea na Ziara.


Mbali na Ziara hiyo Viongozi hao pia wamefunguka kuwa Wakirudi nchini watakuwa na Tour Ya Mikoani kwa ajili ya huduma ambapo ratiba kamili itatolewa mara baada ya kundi hilo Kurejea Kutoka Nchini Kenya.

Blogger wa Blog anawatakia Ziara Njema yenye mafanikio ya kufungua milango zaidi ya nje ya Tanzania.



Mwanamuziki Mwingine Wa GWT Aachilia Albam Yake Sokoni...Loveness Mkama



Baada Ya Mwanamuzi wa Ndani ya Kundi la GWT Paul Clement Kutoa albam yake yenye jina la Umeniita mwanamuziki Mwingine ndani ya Kundi hilo la Glorious Worship Team Loveness Mkama ameiachilia Sokoni albam yake yenye jina la "Wamtumainio Bwana" albam hiyo inanyimbo 10.

Mwanamuziki huyo ameiambia blog hii kuwa Albam yake hiyo ili i-record mwaka 2008 na haikuwa sokoni kutokana na sababu kadha wa kadha isipokuwa mwaka huu wa 2013 Mungu alipenda ndio iingie sokoni na anategea kuiweka kufanya Video Recording Ya Albam hiyo baada ya siku chache zijazo.


Loveness Mkama amemwambia Ze Blogger kuwa kimsingi hii ni Albam yake ya tatu tangu aanze kufanya kazi za muziki wa Injili akiwa Arusha enzi hizo. Mwanamuziki huyo mwenye ndoto za kutengeneza Albam yake ya Live na Kumiliki Kundi lake la Muziki wa Injili na Kucheza Filamu amesema amefungua mlango kwa wasambazaji wa kazi za Muziki wa Injili ndani na Nje ku-sign na Mikataba ya Usambazaji kupitia Meneja Wake na Mwanasheria anayesimamia Usambazaji wa Kazi zake za Injili hapa Tanzania.

Blogger alitaka kufahamu kama bado ni Mwanamuziki wa Glorious, alijibu kuwa hajajitoa katika Kundi hilo yeye bado ni mwanamuziki wa kundi hilo na albam hiyo aliitoa kabla hata hajajiunga na kundi hilo.

Wazungu Wajitoa Kusaidia Kituo Cha Watoto Yatima Kwa Sababu Ya Kulitaja Jina la Yesu

Chomoza Wiki Hii Ilifunga Safari Katika Wilaya Ya Mkuranga Mkoa Wa Pwani Kwenda Kupata Ukweli wa tetesi kuwa Kuna Wazungu Wameamua Kurudi Kwao Baada ya Kuwataka Viongozi wa Kituo Cha Kuwatunza Watoto Wanaoishi Mazingira Magumu Cha Hananasif Kulitaja Jina la Yesu.

Safari Ya Chomoza Ilianzia Kwenye Ofisi Za Clouds Mnamo Saa 1 na Nusu Asubuhi na Kwa Mwendo wa Wastani timu ya Watu Watano Ilikuwa ikielekea Mkuranga Kwa ajili ya Kwenda Kupata Ukweli wa Habari hiyo. Mara baada ya Kufika Mkuranga Majira ya saa 3 asubuhi timu ilipokelewa na Mkurugenzi wa Kituo hicho pamoja na Walimu wanaofundisha katika Shule hiyo. Na ndipo Habari Kamili ikaanza kuelezwa na Mkurugenzi wa Kituo.

Mkurugenzi Wa Kituo Cha Hananasif alieleza kuwa kituo cha Hananasif ambacho kimejenga shule yake yenye jina la HOCET ambapo imekuwa ikiwatunza watoto hao na kuwasomesha kuanzia form one mpaka form four kisha wanafunzi hao hupata fursa ya kuendelea na masomo ya A level na mpaka chuo. Mkurugenzi huyo alieleza kuwa kwa sasa kuna watoto zaidi ya 11 ambao kupitia kituo hicho wameweza kufika elimu ya Chuo Kikuu na Vyuo Vingine. Pia alieleza Kituo hicho kina Mradi wa Kuku ambao kwa sasa umesimama kutokana na sababu mbalimbali lakini wanayo machine ya kisasa ya Kutengeneza Mayai ambayo mayai hayo  yatakuwa yakiuzwa yataiingizia fedha Kituo hicho kwa ajili ya kuhudumia Watoto wanaotunzwa kituoni hapo. Mbali na Mradi huo wa Kuku, Pia timu Ya Chomoza ilishuhudia Ng'ombe Wasiopungua 10 ambao wanatoa maziwa katika shule hiyo ambapo sehemu ya maziwa wanatumia wanafunzi hao lakini sehemu nyingine ya maziwa inauzwa kwa ajili ya kuendeshea kituo hicho. Mbali na Mradi wa Ng'ombe pia Kituo Pia Kilishuhudia Ulimaji wa Bustani ya Mboga mboga ambazo Wanafunzi wa Kituo hicho wanalima kwa ajili ya kungunguza gharama za ununuaji wa mboga kila mara ambapo kupitia kituo hicho wanafunzi wamefundishwa namna ya uzalishaji wa Kujitegemea ili kumudu gharama za uendeshaji wa kituo hicho chenye jumla ya Wanafunzi 96 kwa sasa. 

Mbali na Shughuli za Uzalishaji Pia Chomoza Ilishuhudia Maabara inayotumika na shule hiyo kwa ajili ya Masomo ya Sayansi na pia timu ilishuhudia studio ndogo ya kienyeji ambayo wanafunzi wa shule hiyo wanatumia kama sehemu ya kukuza vipaji vyao vya uimbaji.

Mkurugenzi Wa Hocet, Mwalimu Mkuu wa wa Kituo hicho na Wanafunzi walipoongea na Chomoza wanaeleza kuwa Wazungu waliokuwa wakisaidia shule hiyo kwa michango yao walishindwana na Uongozi wa Kituo hicho katika mambo kadha wa kadha mojawapo likiwa la Kuwataka Wanafunzi na Watoto wa Kituo Hicho Wasiwe Wanataja taja Jina la Yesu. Chomoza Ilipotaka Kujua Kwanini Wazungu Waondoke kwa sababu hiyo walieleza kuwa Wazungu walisema huko kwao wanakotoa fedha sio wote wanamjua Mungu na Kusali inakuwa sio fair kwao wao wasioamini katika Mungu. Management na Wanafunzi wakakataa sharti hilo Wazungu wakajitoa katika Mpango mzima wa kusaidia Kituo Hicho.

Kati ya Changamoto wanazokabiriana nazo tangu Wazungu wajiondoe katika kituo hicho ni ufumo wa upatikanaji wa Chakula kwa ajili ya Watoto hao. Pia tatizo la Visima Vya Maji ambavyo vinahitaji kufufuliwa ili kuweza kuendelea kutoa maji lakini pia wanahitaji gari aina ya canter kwa ajili ya kusaidia kituo hicho. Jumla ya fedha ili kituo hicho kiweze kuboresha miradi yake ya kuku, ng'ombe na kilimo, visima vya maji, machine ya kukatia kuni pamoja na gari inahitajika jumla Ya Milioni 20 ili kuwatengenezea Mfumo wa Kujiendesha na kuepukana na manyanyaso ya Wazungu.

Blog hii pamoja na Kipindi Cha Chomoza kwa kushirikiana na Watu Wachache tunakusudia kuandaa tamasha la Hisani la Kukusanya fedha jumla ya Mil 20 kwa ajili ya Kuwatengenezea mfumo wao wa fedha kuachana na utegemezi. Siku ya tarehe 23 June, 2013 litaandaliwa Tamasha maalum la Kuchangia Watoto hao. Kama unataka tembelea Kituo ama kuchangia Chakula kwa Watoto hao ama Msaada wowote tfadhari Wasiliana nasi kwa 0713 494110 ama chomozashow@gmail.com. Mungu akizungumza na wewe jambo tushirikiane sasa na hata baadae.

Story Kamili Ya Kituo Na Mahojiano Usikose Tazama Chomoza, Siku Ya Jumapili Saa 12 jioni katika Segment Ya Kwataarifa Yako.


 Timu Ya Chomoza Ndani Ya Ofisi Ya Walimu
 Usifanye Mchezo na "White Balance" Unapofanya Interview ya Mtu Mweupee na Mweusiiiii, Papaa akimuwekea White Balance Noel Tenga
 Mojawapo Ya Kisima Kinachotumiwa na Wanafunzi wa HOCET 
 Kazi Haikuwa ya Kitoto hapa tulikuwa tunaenda kwenye Mabanda Ya Ufugaji
 Tukikaribia Mabanda
 Humu Kuna Ng'ombe Wa Maziwa
 Mojawapo ya Ng'ombe
 Hapana Chezea Kuchoka
 Wakati Wa Kurudi Gari Likakwama kwenye Mchanga
 Hapa Sasa Shide Ikahitajika Kweli hii Kazi
 Full kazi
 Camera Man wa Chomoza Haruni Kuhani tangu enzi za Amana Vijana Centre miaka hiyo.
 Baadhi Ya Walimu Wakifatilia issue nzima ndani ya ofisi
 Timu Ya Chomoza, Papaa, Noel Tenga na Jimmy Tukichora Plan ya Kazi baada ya kufika eneo la tukio
 Kazi Ikaanza namna hii James Temu akiwa na Mkurugenzi Mr. Mwalugaja mbele ya Camera Man Haruni.
 Mtu Mzima akitiririka ndani ya Kipindi
 Sijui Mwalugaja alikuwa analia??sikumbuki vizuri ila Jimmy alikuwa anaongea baada ya Mwalugaja Mkurugenzi wa Kituo Kuongea sakata la Wazungu.
 Chomoza Ikienda Saawa na Mkuu wa Chuo juu ya Changamoto za Wazungu
Chomoza Ikienda Sawa na Wanafunzi.


Chomoza Ikienda sawa na Noel Tenga kuhusu Kuandaa Tamasha la Kukusanya fedha kwa ajili ya watoto hao.
Timu La Chomoza Kushoto Papaa, Noel Tenga, James Temu na Camera Man Haroun.


Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...